
TAMKO::
Kwa kuwa tunatambua kwamba sayansi ya jamii:
- ni elimu inayohusu ya jamii
- ni elimu inayohusu maisha ya watu, makundi ya watu, na jamii yote.
- ni elimu inayohusu tabia na mienendo ya mwanadamu, katika Nyanja zote katika mahusiano, mazingira na maisha ya kila siku, kuanzia kwenye kaya, mtaani, dunia nzima.
- ni elimu inayohusu mambo yote yanayoigusa jamii huku yakimuhusu mwanadamu katika maisha yake yote, urefu wa uhai wake, na hata baada ya uhai wake.
- ni elimu inayogusa na kuunganisha elimu na maarifa yote yanayomhusu mwanadamu
Kwa hiyo sisi wanachama wa taasisi ya sayansi ya jamii tunaamua kuanzisha taasisi hii ili kuweza kutafasiri kwa vitendo malengo ya sayansi ya jamii katika jamii yetu ili kujenga jamii inayojitambua, inayotambua tunu zake, iliiweze kuzitumia tunu hizo kuondoa umaskini, na kujenga jamii yenye maelewano, maendeleo endelevu, na ustawi.